Monday, September 18, 2023

NINA MAFUTA YA KUONDOA MAKUNYANZI

Rejuvenating cream inaondoa mikunjo kwenye ngozi yako ya uso na mikono ili kukurejesha katika muonekano wa ujana.
Bei 115,000


Piga au Whatsapp 0755200023

Thursday, September 14, 2023

LOTION YA KUONDOA MAKOVU, WEUSI NA ALAMA NYEUSI



BODY LUV
imekamuliwa kutoka kwenye mafuta ya mimea, Hii bidhaa ni nzuri ,hasa hasa kwenye zile sehemu zinazoshika weusi Kwa haraka.. mpajani, sugu zote, kwapani, na wale wenye makovu sehemu yoyote.
 
πŸ“Œ MATUMIZI unaipaka kabla ya kuoga sehemu zenye weusi unakaa nayo dakika 5  baada ya hapo unaenda kuoga na kuacha sehemu ya weusi ikiwa Laini .. 
πŸ“ŒPia Ina harufu nzuri na hainati inasambaa yenyewe Tena Kwa urahisi inapokutana na maji 
πŸ“ŒInazuia ukavu wa kukatika Kwa ngozi haswa magaga na kuacha ngozi yako ikiwa laini

Call/watsp
0628645231 au 0755200023
@_neolife_tip

Njoo Kuna Fursa ya Vipodozi na Bidhaa za Afya na Usafi

Nina Fursa. πŸ’•
Njoo Whatsapp 0755200023




TUNAHITAJI MAWAKALA
Na PIA TUNAUZA BIDHAA KWA BEI YA KAMPUNI

MAWAKALA MTAJI NI 370,000/=

WANUNUZI WATAPEWA BEI ELEKEZI WATSP

CALL/WATSP
0628645231
@_neolife_tip

Thursday, July 27, 2023

MAMA BEYONCE AOMBA TALAKA NDOA YA PILI



Mama yake #Beyonce, Tina KnowlesLawson (69) ameomba talaka kuvunja ndoa yake ya mara ya pili ili aachane na mumewe Richard Lawson (76).

Kwa mujibu wa nyaraka za kisheria zilizopatikana na mtandao wa TMZ, Tina ameanza mchakato wa kuomba talaka jumatano iliyopita.

Kwenye nyaraka hizo inaripotiwa Tina ameainisha sababu ya kutaka kuvunja ndoa ni tofauti zisizorekebisha pia ameomba baada ya talaka mahakama imrejeshee jina lake la mwanzo Celestine Knowles na pia kusiwe na matunzo ya mwenza (spousal support).

Ndoa ya Tina na Richard ina miaka 8, walioana 2015 ndoa iliyofanyika kwenye boti huko California na waalikwa wote walivalia white si baadhi yenu mnakumbuka mapichapicha eeh.

Mara ya kwanza Tina aliolewa na baba yake Beyonce, Mathew Knowles toka 1980 hadi 2011 na wakafanikiwa kuzaa mabinti wawili Beyonce na Solange.

Ndoa ya baba na mama Beyonce ilivunjika baada ya kugundulika Mathew wakati huo akiwa meneja wa kundi la kina Beyonce la Destiny's Child kazaa nje ya ndoa na muigizaji Alexandra White mtoto wa kiume anayeitwa Nixon Knowles aliyezaliwa 2010.

Awali Mathew alikataa Nixon sio mwanae lakini baadaye vipimo vya DNA ikathibitika ni mwanae.

Ndipo ndoa ya mama na baba Beyonce ikavunjika kwa mama Beyonce kuomba talaka na baada ya hapo kila mmoja akafunga ndoa mpya ambapo baba Beyonce alimuoa modo Gena Charmaine Avery toka 2013 hadi leo wako pamoja.

Wiki chache zilizopita Alexandra amehojiwa na jarida la Uingereza la the sun akasema mwanae Nixon hana ukaribu na dada zake (kina Beyonce na Solange) wala baba yake (Mathew Knowles).
Yani familia ya Knowles haitaki kujihusisha na Nixon.






Tuesday, July 25, 2023

HASIRA ZIMECHANGIA KUVUNJA NDOA YA DULLA MAKABILA



Kuhusu waliokua wanandoa #DullaMakabila na #Zaiylissa kuachana; Zaiylissa amefunguka " Nimemuacha kwasababu nimechoka, hajatulia na ana hasira sana".

Zaiylissa amesema ni kweli amepewa talaka 3 kwa mpigo ambazo Dulla aliziweka kwenye bahasha na zikawasilishwa nyumbani kwa Zaiy Chamanzi.

Akielezea maisha ya ndoa kwa miezi miwili na siku 10 alizoishi na Dulla; Zaiy amesema Dulla alikua na matukia ya rejarejaja yasiyo na kikomo ikiwemo kumfumania na meseji za warembo wa mjini na akimhoji anaambulia kipigo.

" Sio rahisi kuishi na Dulla kwa ajili ana kashkashi nyingi na hata wakati naolewa baadhi ya ndugu zake waliniita pembeni na kunisihi Dulla hajatulia niwe naye makini", ameeleza Zaiylissa, akaendelea kusema kuwa amejitahidi sana lakini uvumilivu umemshinda ameamua kuchapa lapa na kusepa.

Zaiylissa akaendelea kufunguka kuwa tokea awe kwenye mahusiano na Makabila hakuwahi kuchepuka hali ambayo hadi mume alimuuliza mbona huchiti maana kila akipekua simu hakutani na sintohamu yoyote.

Zaiylissa akamalizia maelezo yake kwa kusema kingine kilichofanya ndoa na Makabila imshinde ni kwamba Dulla ana hasira sana ambazo mara zote ziliishia mwilini mwa Zaiy kwa kipigo.

Monday, July 24, 2023

NDOA YA DULLA MAKABILA IMEVUNJIKA



Nyota wa muziki wa Singeli Tanzania mwanamuziki Dulla Makabila amekiri kuwa ndoa yake na muigizaji wa tamthilia ya juakali Zaiylissa imevunjika.

Tetesi za kuvunjika ndoa hiyo zilianza mwanzoni mwa wiki iliyopita baada ya mkewe kuondoa picha zao zote za pamoja na kumu unfollow mumewe kwenye account ya instagram.

Leo julai 24, 2023 Dulla akihojiwa na kipindi cha radio kwa njia ya simu amekiri ni kweli ndoa hiyo imevunjika.

Aidha kuna picha na video zinazomuonyesha Zaiylissa akiwa na vidonda vibichi vinavyochuruzika damu ikiaminiwa vimetokana na kipigo toka kwa ex wake.

Dulla na Zaiylissa walifunga ndoa may 12. 2023.
Ndoa ambayo imedumu kwa miezi miwili.

Miaka ya nyuma wote walishafunga ndoa na wapenzi wengine ambazo nazo zilivunjika.

Kwa Matangazo wasiliana na 0755200023.

MCHEKESHAJI JAYMONDY ANADAIWA KUMTELEKEZA MWANAE BAADA YA KUPATA GIRLFRIEND MZUNGU



Mchekeshaji #Jaymondy anadaiwa kutelekeza mtoto kisa kapata girlfriend mzungu.

Akieleza kwa uchungu mzazi mwenza wa mchekeshaji huyo amesema kipindi cha nyuma Jaymondy alikua anatoa matunzo ya mtoto na hata wao kama wazazi walikua na mawasiliano mazuri; lakini baada ya mzazi mwenzie huyo kupata mzungu mambo yamebadilika kabisa.


Baby mama huyo amesema mpasuko kati ya mzazi mwenzie na wao (mama na mtoto) ulianza kutokea baada ya Jaymondy kupata mzungu.
"Mapenzi yameisha kabisa kwa mtoto na hata hakumbuki ni lini kamjulia hali mtoto".
"Mtoto amefukuzwa shule ada na baba yake anaonekana mitandaoni akila raha Ulaya na hata alivyoondoka hakumuga mtoto", amesema baby mama wa Jaymondy.

Baby mama akaendelea kueleza kwa uchungu;

"Mzungu amefunga kila sekta hakuna mawasiliano kabisa."

Kwa sasa Jaymondy anaishi Scandinavia na mwanamke wake mzungu.

Saturday, July 22, 2023

TRACY NABOKERA NDIYE MSHINDI WA MISS TANZANIA 2023



Kampuni ya The Look chini ya Miss Tanzania Organization jana julai 21, 2023 imemtangaza mlimbwende Tracy Nabokera kuwa ndiye mshindi wa miss Tanzania 2023.

Kutangaza Biashara yako hapa wasiliana na 0755200023

SALUNI YENYE MANDHARI NZURI YA KUCHA NA NYWELE MWENGE DAR ES SALAAM

Je unatafuta salon yenye mandhari nzuri, safi na tulivu kwa ajili ya kusuka nywele zako na kutengeneza kucha?

Njoo Mwenge Mwenge Salons

OFFER RANGI YA GEL *5,000 NA KUBANDIKA KUCHA NA GEL *10,000*                             ☎️0787595342.                                 πŸ’…πŸ½πŸ’…πŸ½πŸ’…πŸ½ *At Glow & Beauty*

@mwenge_salons  #glow & beauty

Ghorofa ya kwanza - Jengo la Jamirex MWENGE SOKONI - Juu ya AZANIA BENKI.                      
                                                             
*Parking zipo za kutosha*

πŸš™ 🚘 



@mwenge_salons …. AT-GLOW & BEAUTY πŸ’…πŸ½πŸ’…πŸ½πŸ’…πŸ½




Karibuni sana πŸ™πŸ™πŸ™ πŸ’…πŸ½πŸ’…πŸ½πŸ’…πŸ½










#gelnails 
#nails 
#tanzania                 #daressalaam 
#mwenge 
#naturalhairstyles        #makeup                           #kucha                            #kusuka            #nywelezamkono             #cornrows                           #twist.                              #crochet                                 #rasta                  #jamirexhotelmwenge

@mwenge_salons 
@vivimachangeblog

Thursday, July 20, 2023

WANANDOA PRINCE HARRY NA MEGHAN MARKLE WANADAIWA KUTENGA MUDA KUISHI KILA MMOJA KIVYAKE

Ripoti mpya kutoka mtandao wa #RadarOnline inadai kuwa wanandoa #PrinceHarry na mkewe #MeghanMarkle wamejipa likizo kila mmoja anaishi kivyake kwa sasa wakijitafakari ni hatua ipi ifuate katika ndoa yao baada ya misukosuko iliyotokana na madili yao kufeli.

Msongo wa mawazo kati yao unaripotiwa kuanza baada ya kukosa dili la $ milioni 20 spotify na podcast yao Archetypes kushindwa kupata msimu wa pili, chanzo kimesema.

Vyanzo kutoka familia ya kifalme vinaamini Harry anajaribu 'kujitafuta'  baada ya mabadiliko mengi toka aondoke kwenye kasri.
"Wanajitahidi kujitafakari ni nini kimewagonga', chanzo kimefunguka.
" Harry hafiti kwenye mishe za ulimwengu wa Meghan."

Aidha vyanzo hivyo vimeuambia mtandao wa Radar kuwa Harry ana tripu ya kwenda Afrika kufilimu dokumentari yake ya Netflix kwahivyo vinaamini safari hiyo itamuonyesha picha ya hatua inayofuata kwenye ndoa yake.

Safari hiyo ya Harry pekee inatarajiwa inaweza kuwa ndio kitu Harry anahitaji kwa ajili analichukulia bara hilo kama "nyumbani kwake kwa pili na mahali ambapo anajisikia zaidi kuwa yeye", chanzo kimesema.

" Kutawanyika kila mmoja bara tofauti inatarajiwa kuwasaidia kuona ni namna gani wasonge mbele."

Wakati huohuo vyanzo vimesema Meghan tayari ana wakala bomba kwa kum brandi, "anataka ajirandi yeye kama yeye atengeneza mamilioni", mtaalam wa maswala ya kifalme Daniela Elser amesema. "Ni kwa mara ya kwanza kila mmoja anajijenga kitaaluma kwa njia yake."

" Meghan na Harry wapo kwenye presha kubwa kifedha ili kuishi maisha ya kifahari ya California ikiwa ni pamoja na jumba lao la dola milioni 14 pamoja na ulinzi wa hali ya juu", chanzo kimesema.

Ndoa ya miaka mitano ya Prince Harry na Meghan Markle imepitia kashkashi nyingi zikiwemo baadhi ya media kubwa za Uingereza kuwakeka kwenye picha hasi, kuhamia California na kuachana na majukumu ya kifalme na kufunguka kwa kina hadharani mambo hasi waliyopitia kama wanandoa kwenye familia ya kifalme.




Nifollow instagram @vivimachangeblog

Kutangaza Biashara yako hapa wasiliana 0755200023


Tuesday, July 11, 2023

WALIO KISS MOI

Juzi jumapili julai 9, 2023 mchana video ilisambaa mitandaoni ya mgonjwa aliyekua amelazwa wodini katika hospitali ya Muhimbili akila denda na mwanamke.

Menejimenti ya Tiba ya Mifupa ya hospitali hiyo MOI imetoa ufafanuzi kuhusu uvunjifu wa maadili ya Kitanzania uliofanywa na mgonjwa huyo jina limehifadhiwa aliyekua amelazwa wodi namba 3A.

Mgonjwa amekiri kufanya kitendo hicho na mwanamke aliyedai ni mpenzi wake.

Kama ilivyodhaniwa na wengi wa waliotazama video hiyo ya kwamba mwanamke huyo ni muuguzi; MOI imebaini sio muuguzi wala mfanyakazi wa MOI na kwamba video ilirekodiwa na mgonjwa wa pembeni na tendo la denda kuendelea lilikatishwa na muuguzi wa zamu.

MOI inalaani na kukemea kitendo cha kurekodi video wodini na kuisambaza mitandaoni pia kitendo mgonjwa aliyekula denda kuvunja maadili ya Mtanzania kwani ni kinyume na miongozo ya wizara ya afya.

Aidha mgonjwa huyo pia
amewaomba msamaha Watanzania.



NiFollow instagram @vivimachangeblog

Kwa MATANGAZO ya Biashara nicheki 0755200023


DIVA AMETANGAZA KUACHANA NA MUMEWE

Mwanahabari mtangazaji wa media ya Wasafi Diva Malinzi aka Diva the bawse ametangaza kuachana na mumewe Sheikh Abdulrazak Salum.

Diva amesema Abdulrazak ambaye ni mtaalam wa mahusiano kupitia visomo vya dini ni mpigaji, muongo na mnyanyasaji na amewaonea huruma wateja wake (wa Abdul).

Diva anasema Abdul amemtesa sana kwa kipindi cha ndoa yao ya mwaka na nusu.

Diva aliwahi kusema Abdul ana watoto watano aliozaa na wanawake wengine mbalimbali na alijitolea kwa moyo mweupe kuwa mama yao wa nyongeza.

Nifollow instagram @ViviMachangeBlog

Kwa Matangazo ya Biashara nicheki 0755200023



Monday, July 10, 2023

BARNABA NA RAYA WAMEFUNGA NDOA

Mwanamuziki wa bongo fleva Barnaba na mpenzi wake wa muda mrefu Raya wamefunga ndoa.

Barnaba ambaye alibadili dini kufuata ya Raya sasa anaitwa Mohamed.

Kamati imezawadia shilingi milioni 2.

Raya mjasiriamali wa saluni ya kike ni mtoto wa muigizaji machachari Mama Kimbo.

Mama Kimbo akitoa nasaha zake amesema amefurahi sasa kuwa mkwe halali.

Kwa hadharani hii ni ndoa ya mara ya pili kwa Barnaba ambapo awali alimuoa mrembo Zuu Namela ndoa ambayo baadaye ilivunjika.

Barnaba na Zuu wamejaliwa mtoto mmoja anayeitwa Steve.

Barnaba na ex wake Zuuh wana mahusiano mazuri na wanashirikiana malezi ya Steve ambapo Raya naye mara nyingi anashea mitandaoni akiwa na mtoto wake wa faida Steve.

Nifollow instagram @ViviMachangeBlog

Kwa huduma ya Matangazo wasiliana nami namba 0755200023

Sunday, July 9, 2023

PADRE AMEFARIKI ASUBUHI BAADA YA KULALA USIKU MZIMA NA KIPENZI CHAKE HOTELINI



Padre wa Kanisa Katoliki parokia ya St Peters Ruai nchini Kenya amefariki baada ya kulala na mpenzi wake usiku mzima hotelini huko Murang'a.

Padre huyo ambaye ametambulika kama Joseph Kariuki Wanjiku (43) amefariki jana asubuhi julai 8 baada ya kukimbizwa hospitali na mpenzi wake akishirikiana na baadhi ya wafanyakazi wa hoteli waliyokuwemo.

Ripoti ya polisi inasema wapendanao Joseph na kipenzi chake (32) waliingia hoteli ya Monalisa Delview Gatanga ijumaa jioni.

Padre akaanza kujisikia vibaya jumamosi asubuhi.

Mpenzi wa Joseph mwanadada ambaye jina limehifadhiwa naye anafanya kazi katika parokia aliyokua anahudumu padre Joseph.




Follow @vivimachangeblog

MATANGAZO 0755200023

Saturday, July 8, 2023

CCM Imemfukuza Uanachama Balozi Ali Karume



Halmashauri Kuu Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Kusini Unguja imemfuta uanachama kada wake Balozi Ali Karume.

Taarifa ya kumuondoa kwenye chama imetolewa na katibu mwenezi wa mkoa huo Ali Timamu Haji kutokana na kikao kilichofanyika saa saba usiku wa kuamkia leo julai 8, 2023 chini ya Katibu wa CCM wa mkoa Amina Mnacho.

Hatua hiyo inakuja baada ya CCM kumpa onyo kutokana na kauli zake akidaiwa kukidhalilisha na kuwatukana viongozi wakuu hadharani.

Nifollow so @ViviMachangeBlog

Tangaza Biashara yako hapa wasiliana na 0755200023

Wednesday, July 5, 2023

MWANAFUNZI WA UHASIBU MTWARA AMEJIUA KWA KUJINYONGA, AMEAGA STATUS KWA PICHA YAKE YA ZAMANI

Mwanachuo wa Uhasibu TIA mkoani Mtwara anayefahamika kwa jina moja la Reagan amejinyonga kwa kujiua ikihisiwa ni baada ya ugomvi na mpenzi.

Mwili wa Reagan aliyekua akiishi mtaa wa Chikongola Mikindani umekutwa ukining'inia chumbani kwake Jana July 4, 2023.

Baadhi ya mashuhuda wamesema,

" Huenda Reagan aliamua kujiua kisa mapenzi kwasababu siku sio nyingi aligombana na mpenzi wake waliyekua wanaishi pamoja."

Kamanda wa polisi Mtwara Nicodemus Katembo amethibitisha kupokea taarifa za tukio hilo na kusema atalitolea ufafanuzi
baada ya ripoti ya uchunguzi wa madaktari kukamilika.
Mwili wa Reagan umehifadhiwa hospitali ya rufaa ya mkoa ya Ligula.

Muda mfupi kabla ya marehemu Reagan kujinyonga aliweka ujumbe whatsapp status akiuambatanisha na picha yake ya utotoni uliosomeka 'kwa jasho lako utajipatia chakula hadi utakaporejea mavumbini ulimotwaliwa, MAANA WEWE NI MAVUMBI NA MAVUMBINI UTAREJEA'.

Nifollow instagram @vivimachangeblog

Tangaza hapa wasiliana nami kwa 0755200023

CHEKA



Utakaa hivi ikiwa unamuendesha mama mkwe?🀣

Tangaza Biashara yako hapa wasiliana nami kwa 0755200023

Nifollow instagram @vivimachangeblog

Mama mkwe wa Beyonce “ameoa”



Gloria Carter mama mzazi wa rapper mkongwe Jay-Z amemuoa mpenzi wake wa muda mrefu mwanadada Roxanne Wilshire jumamosi iliyopita jijini New York nchini Marekani.

Miongoni mwa waliohudhuria harusi hiyo ni mwali wake Beyonce , mjukuu wake Blue Ivy ambaye ni mtoto wa kwanza wa Beyonce na Jay-Z pamoja na mama wa Beyonce Tina Knowles Lawson.




Gloria amejaliwa kuzaa watoto wanne wakubwa wa kiume kabla hajajitangaza kuwa ni msagaji.

Tokea ajitangaze kuwa ni mpenzi wa jinsia moja mwanae bilionea Jay-Z amemuunga mkono mama yake kwa asilimia 100.

Nifollow Instagram @vivimachangeblog

Monday, March 14, 2022

Mama Diamond Azima Kelele za Kuwa Hapendi Mahusiano ya Mwanae na Zuchu

Ingawa ni muda kiasi toka kumekuwepo na gumzo mitandaoni ya tetesi za mahusiano ya mapenzi kati ya Diamond Platnumz na msanii wake Zuchu, baada ya kutoka kwa wimbo wa Mtasubiri ambao Diamond kaimba kwa kumshrikisha mwanadada huyo uliopo kwenye EP FOA ya Diamond wadau wanaona ni kama umethibitisha tetesi hizo.

Wawili hao wamezungumziwa sana kuhusu mahusiano ya mapenzi yaliyodaiwa kuwepo huku mashabiki wengi wakiamini kwamba wimbo huo umethubitiaha uwepo wa penzi.

Wadau wa mitandaoni wakawa wanadai Diamond anashindwa kujiachia kwa kipenzi chake Zuchu kwa kuweka mambo peupe kwa ajili anamuogopa mama yake almaarufu Mama Dangote kwa ajili tetesi zinadai hayapendi mahusiano hayo. 

Na tetesi hizo zikapaliliwa zaidi na kitendo cha Mama Dangote kutom follow instagram msanii huyo wa kike pekee kwenye lebo ya mwanae.

Leo jumatatu March 14 Mama Dangote amepost video ikimuonyesha Diamond na Zuchu wakiimba wimbo wa Mtasubiri ambapo wadau wa mambo wanatafsiri kama ni ameamua kukata mzizi wa fitna.

Mdau nini maoni yako je kwani kuna nongwa yoyote endapo mzazi anaingilia penzi la mwanae?

Saturday, March 12, 2022

Nuh Mziwanda Aomba Pambano la Ngumi na Shilole

Baada ya mwanadada Shilole kutamba kumtembezea kipigo mume wake wa zamani Nuh Mziwanda iwapo atazidi kumfuatilia, naye Nuhu amevunja ukimya kwa kuomba pambano na mke wake huyo wa zamani.

"Manake hapo kwanza ncheke, Mziwanda mimi au mwingine? naomba pambano viwanja vipo vingi tu nikuonyeshe show mama Ntilie. Kwanza nina hasira na wewe ulinipiga Leaders club ukijichanganya tu nakufumua vibaya sana," aliandika Nuhu

Kwenye mtandao wa instagram mara kadhaa Nuhu amekuwa akimtuhumu Shilole ambaye kwa sasa ni mke wa mpigapicha Rommy 3D, pia mwanamuziki na mfanyibiashara ya kupika chakula kuwa alikua anajihusisha na mambo ya kishirikina enzi ya penzi lao.

Friday, March 11, 2022

Kuhusu Diamond Kumuoa Zuchu Haiwezekani - Sallam

Siku ya jana kwenye uzinduzi wa EP ya Diamond Platnumz meneja wake Sallam alitoboa siri kwamba Diamond na Zuchu hawawezi kuoana kwasababu wao wanafanya biashara na Diamond ni boss wa Zuchu.

Ishu nzima ilianza hivii: Wakati Diamond alipokuwa anatumbuiza kwenye ngoma yake mpya ya Nawaza, katikati ya tukio meneja wake Bwana Salaam akasema kila mtu atoe dukuduku lake aseme anawaza nini. Ndipo kaka wa Diamond, Romy Jons akachomekea kuwa nawaza Diamond atamuoa Zuchu na ndipo Sallam akajibu kwamba haiwezekani kwasabbau yeye Diamond ni bosi na wanafanya biashara.

Skendo kwenye Ep Ya Diamond Nawaza Kutishia Ndoa Ya Lulu na Majizzo?

EP mpya ya Diamond Platnumz FOA aliyoiachia usiku wa jana kuamkia leo imeibua skendo ya kuwepo kwa clipu za mapenzi kati ya Elizabeth Michael "Lulu" na Rayvanny hali iliyopelekea maswali mengi kwa mashabiki.

Wakati huohuo Majizzo ambaye ni mume wa Lulu kafuta posts zake kwenye ukurasa wake wa instagram akizokua amemsifia mkewe huyo ikiwemo ile ya siku ya wanawake na ya anniversary ya mwaka mmoja wa ndoa yao.

"Nawaza Vanny na Eliza clip zao zikivuja, ndoa itaimarika eti au wataivunja?" hii ni vesi iliyozua gumzo.

Aidha pia kuna baadhi ya video zinazosambaa kwenye mitandao zinazoonyesha kuwepo kwa uhusiano wa karibu kati ya Lulu na Ray.

Thursday, March 10, 2022

Ufafanuzi wa Hospitali ya Muhimbili Kuhusu Kusambaa Video ya Mgonjwa Profesa Jay

Hospitali ya Taifa ya Muhimbili imetolea ufafanuzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Joseph Haule maarufu Profesa Jay na kusema kuna video inayosambazwa na mtandao wa Mange Kimambi ikimuonesha Profesa Jay akipatiwa matibabu Muhimbili Hospitali Upanga.

Uongozi wa hospitali unatoa taarifa kuwa video hii haijarekodiwa na kusambazwa na hospitali, tumesikitishwa na tunalaani vikali kitendo hiki cha kumrekodi mgonjwa anayepigania uhai wake ICU na kuisambaza, hiki ni kiwango cha juu cha kukosa utu na maadili.

"Tunafuatilia kwa ukaribu tukio hili ili kubaini chanzo cha video hiyo ili hatua stahiki zichuliwe, wananchi endeleeni kuwa na imani na hospitali ya Muhimbili." imeeleza taarifa iliyotolewa an hosptali ya Muhimbili.

Friday, July 16, 2021

HATUA ZA KUTATUA TATIZO ILI UBAKI NA HESHIMA YAKO

 Follow Instagram |@vivinavisavyake

Ukipatwa na tatizo kama unataka ulitatue kwa jinsi ambayo mwishoni utabaki na heshima yako basi fuata hatua hizi.

1. Unapolipokea usihamaki bali lijue tatizo kwa undani na kwa ukweli
2. Fahamu unachotaka kutokana na hilo tatizo.
3. Angalia mifumo iliyopo na uchague utakaoweza kutatua tatizo lako.
4.Fuatilia mfumo uliochagua je unatatua ama unaongeza tatizo.
5. Kama mfumo uliochagua unatatua basi utakupatia suluhisho na kama hautatui badilisha chagua mwingine.
6. Anza kutekeleza suluhisho.

Pia kwa undani zaidi unaweza kufuatilia you tube search Vivi Na Visa Vyake

Thursday, May 6, 2021

NAMNA YA KUEPUKA WIVU

 FOLLOW Instagram @vivinavisa vyake


Ili uweze kuwa na mahusiano mazuri ni lazima ujifunze namna ya kuepuka wivu. 

Kila mtu ameumbwa na wivu tofauti kati ya muonekano wa wivu wa mmoja na mwingine ni ninsi unayemdani hana wivu anavyoweza kuukabili wivu wake na yule unayemuona ana wivu ni jinsi asivyweza kuukabili wivu wake.

Hivyo basi ili kuepuka kuonyesha kiwango cha wivu wajo waziwazi ili hatimaye uwe na furaha na pia na mahusiano mazuri na watu inabidi ufanye yafuatayo:
1. Usijilinganishe na safari ya mwingine maana kila mtu bhapa duniani ana safari yake ya kipekee.
2. Huenda hauko kwenye hatua kama ya unaowaonea wivu kwa ajili |Mungu amekupangia kuna jema lako linakusubiri
3. Muonekano wa wengine unaweza kuona ni mrahisi kumbe hujui stori yao yote.
4. Epuka kufuatilia ya wenzingine maana kunaweza kukuvuruga kazana na kufanya yako.
5. Chagua kuangali na kufanyanya yake yakupayo furaha.

Kama unatatizo linalopelekea kukosa furaha na maendeleo ya nafsi yako njoo tuzungumze simu 0755200023


Tuesday, May 4, 2021

MSHAURI AKIKUPA MAJIBU HAYA NI KWAMBA HANA MSAADA UNAOHITAJI

 FOLLOW INSTAGRAM @vivinavisavyake



Wengi wetu tumeshapitia changamoto za kimahusiano ambapo kumueleza mtu tunayemuamini huwa inatupa ahueni au msaada ambao utatuvusha.

Kama huyo unayemuamini na kumwendea kumueleza anakupa majibu haya ina maanisha kwamba aidha jambo lako ni kubwa sana kwake kuweza kulichakata na kukushauri cha kufanya ama hataki kujishuhulisha nalo.

Hivyo anaweza kukupa baadhi au mojawapo ya sentensi hizi. 
1. Kila kitu kinatokea kwasababu.
2. Liombee tu
3. Muda utasema
4. Achana nalo
5. Usiliongelee tena
6. Utakua sawa ukijaribu kulisahau
7. Acha kulifikiria utajisikia vizuri
8. Kuwa imara tu
9. Maisha ndivyo yalivyo
10. Ambacho hakijakuua kinakufanya imara
11. Ingeweza kuwa mbaya zaidi.

Ukishaona majibu hayo hapo juu, aga tu kwa uzuri na usirejee kwake kwani hutapata msaada unaotaka.
Muhimu ni kwakuwa umeshajua basi usikate tamaa bali tafuta msaada kwingine.

Kama una changamoto ya mahusiano njoo tuzungumze simu 0755200023

 


Tuesday, April 27, 2021

FAHYMA ATANGAZA RASMI KUACHANA NA RAYVANNY: Namna ya Kusonga Mbele Pale Penzi Linapoisha

 follow instagram @vivinavisavyake



Kifo cha mahusiano yaliyokuwa ya maana na ya muda mrefu hakina tofauti sana na kifo cha binadamu. 

Tena unaweza kusema huenda kifo cha binadamu kina angalau kwa kuwa baada ya kuomboleza ni kwamba hautawasiliana wala kumuona tena binadamu huyo duniani. 

Kifo cha mahusiano na mtu ambaye mmezaa kinauma kwa wote wawili yani muacha na muachwa au hata iwe ni kuachana yaani wote kukubaliana kwamba hapa mambo hayaendi tena hivyo tusambaratike tu.

Hivyo basi, inawezekana vipi kusonga mbele baada ya kifo cha mapenzi. Fanya yafuatayo

1. Omboleza. 

Yani omboleza hadi umalize ukitoka hapo ni baibai mbele kwa mbele na maisha

2. Jijenge zaidi kiuchumi. 

Hii itakusaidia kuwa busy na shughuli zako hivyo kutokupa muda wa bure wa kumuwaza mpenzi mlieachana.

3. Usimsema vibaya kwa watu na mbele ya jamii. 

Hii inahusika sana hasa kama mmezaa kwani mnahitaji bado kuwa na mawasiliano na mahusiano mazuri kwa ajili ya mlezi wa mtoto wenu.

Mbinu nyingine njoo tuongee ili uweze ku move on mazima. Simu0755200023

Monday, April 26, 2021

Dida Achumbiwa

follow instagram @vivinavisavyake




Mtangazaji wa kipindi cha mashamsham mrembo Dida Shaibu wa radio wasafi amechumbiwa.

Dida amekua ni mrembo mwenye bahati ya ndoa ambapo ameshapitia ndoa kadhaa kama pia ilivyo kwa watu wengine maarufu mfano Shilole na Hadija Kopa. 

Mdau je, ni muda gani ukiwa na mpenzi ukiona hamvalishani pete utabwaga manyanga?

NIMEREJEA WAPENZI

Nifollow instagram @vivinavisavyake

Hatimaye viblog vyetu na vi you tube vya kupost kazi zetu vimerejea tena. Karibuni tena wapendwa wangu tuyadadavue mahusiano na visa vyake vyote.

Tuesday, October 9, 2018

Ninashona mifuko hii ya kitambaa





Ninatengeneza mifuko hii ya kitambaa kwa vitambaa imara, rangi na ukubwa unaotaka. Hii mikubwa inabeba hadi kilo 10. Bei ni 26,000.
Njoo whatsapp kuchagua design ya kitambaa unachotaka nikutengenezee.
Mawasiliano 0755200023

Table mats za vitenge zipo





Table mats za vitenge kwa design mbalimbali zipo. Pisi 6 ni 30,000
Karibu whatsapp 0755200023

Thursday, October 4, 2018

Michoro na picha za ukutani kuanzia 25,000




Michoro na picha za ukutani kwa ukubwa unaohitaji ipo. Bei kuanzia 25,000
Mawasiliano 0755200023

Batiki na tisheti za batiki zipo





Batiki na tisheti za batiki za kila aina na kwa ukubwa unaotaka zipo. Tisheti bei 15,000
Batiki mita 2 na nusu 17,000
Mawasiliano 0755200023

Foronya za mito ya makochi na kitandani


Tuna foronya za kila aina kwa ajili ya mito ya makochi, sakafuni na kitandani. Bei ni kuanzia sh 7,000. Ukitaka tukushonee kwa vipimo vyako pia inawezekana.
Piga au whatsapp 0755200023 na tunakutumia hadi ulipo.

Friday, August 3, 2018

Muonekano wa wallpaper unapofanana na waTanga Stone

Wallpaper hii ipo. Roll 45,000
Mawasiliano 0755200023

Mito ya makochi


Mito ya makochi aina ya knot pillows ipo. mmoja ni 55,000
Mawasiliano 0755200023

Wallpaper hizi zipo. Roll 45,000





Wallpaper roll moja bei ni 45,000 urefu mita 10 na upana nusu mita. Kama unahitaji na fundi yupo mnaelewana.

Tupo Sinza Mugabe
Mawasiliano 0755200023
Ukitaka kutumiwa whatsapp uchague uletewe inawezekana pia, tunapelekea popote ulipo.
Karibu.